Breaking News

UKRAINE WASEMA INAOUSHAHIDI URUSI KUFYATUA KOMBORA LILILOANGUSHA NDEGE YA MALYSIA

Ukraine imesema inao ushahidi thabiti kuonyesha kwamba waliokuwa wanausimamia mfumo wa makombora uliotumika katika kuiangusha  ndege ya abiria ya Malayasia ni raia  wa Urusi na kwamba lazima wahojiwe.
Hayo ameyasema Mkuu  wa  Ukraine wa kupambana  na ujasusi  Vitaly Nada.
Nada ameeleza kwenye mkutano na waandishi wa habari mjini Kiev   kuwa Ukraine  inao ushahidi  thabiti kwamba kitendo cha kigaidi  cha kuiangusha ndege ya Malaysia kilifanyika kutokana na msaada  wa Urusi. Amesema Ukraine inafahamu fika kwamba mfumo  wa makombora ulikuwa unadhibitiwa na raia wa Urusi.
Wakati huo huo kiongozi wa waasi wa mashariki mwa Ukraine  Alexander Borodai amesema visanduku vya kunakilia safari za ndege ya Malaysia ilioanguka ndani ya Ukraine  havijaonekana.
       

No comments