BIFU LA KEITA NA PEPE HALIISHI LEO WA KESHO
Uhasama wa Real vs Barca ni mkubwa sana kiasi cha hivi juzi nchini Marekani wakati wa mechi ya maandalizi ya msimu mpya kati ya AS Roma dhidi ya Real Madrid, mizimu ya El Clasico iliingilia mchezo huo wakati mchezaji wa zamani wa FC Barcelona Seydou Keita alipokataa kushikana mikono na mchezaji wa Madrid – Pepe na kisha akamrushia chupa ya maji kichwani kabla ya mechi.
Tukio hili lilipelekea wachezaji wengine wa timu hizi mbili kuwatenganisha wachezaji hao, Xabi Alonso akimtuliza mzuka Keita ambae alimtuhumu Pepe kwa kumuita nyani kwenye mchezo wa kwanza wa Spanish Supercopa mwaka 2011.
Kwa mujibu wa Fox broadcast, kamisaa wa mchezo alikaririwa akisema kwamba Pepe alimpiga kibao Keita kwenye ugomvi huo.
Unaweza kuangalia video ya ugomvi wa Pepe vs Keita hapa chini…
No comments